| |
Kuna huduma kwa ajili ya kila mtu Mbezi
Chapel. Kila Jumapili kuna darasa la watoto ambalo watoto
wanapata nafasi ya kuimba, kucheza michezo, na kufundishwa
Biblia na waalimu wanaowapenda. Pia kila Jumapili jioni kuna
mkutano wa vijana ambao vijana wanapata nafasi ya kuabudu,
kujifunza nyimbo mpya, kucheza michezo ya ndani na nje, na
kusikiliza mafundisho yawezayo kuwatia moyo na kuwajenga katika
maisha yao.
Mara kwa mara akina mama
wanakuwa na mikutano maalum kwa ajili yao. Katika mikutano hiyo
wanashirikiana pamoja, kutiana moyo, kuomba na kujifunza Neno la
Mungu. Wazee nao wanapata nafasi mara kwa mara kukutana pamoja
kwa ajili ya mafundisho, maombi na kushirikiana.
Licha ya huduma za
kawaida, kila mwaka kuna kambi, semina, sinema, na mengineo ili
wote wapate nafasi ya kuhudumiwa vizuri na pia kuwakaribisha
wengine kanisani kwetu. |
|