| |
IMANI YETU
KUHUSU MUNGU
Twamwamini Mungu mmoja, wa milele, aliye muumba na mtawala wa
ulimwengu, aliye nafsi tatu, Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu.
Mwanzo 1:1; Zaburi 90:2; Mathayo 28:19; Yohana 10:30; 1 Petro
1:2; Warumi 8:9-11; 2 Wakorintho 13:14
Rejea
KUHUSU YESU KRISTO
Twaamini kwamba Yesu Kristo alizaliwa na bikira Mariamu kwa
uwezo wa Roho Mtakatifu, na kwamba Yeye ni Mungu kweli na
mwanadamu kweli. Twaamini kwamba Bwana Yesu Kristo alikufa kwa
ajili ya dhambi zetu akiwa dhabihu kamili kwa dhambi zetu.
Alizikwa, akafufuka siku ya tatu akishinda mauti na dhambi.
Akapaa mbinguni mahali aliko mkono wa kuume wa Mungu, naye
atarudi duniani ili kutawala kama Bwana wa mabwana na Mfalme wa
wafalme.
Mathayo 1:18-25; Isaya 9:6; Yohana 1:1-5; 14:10-30; Waebrania
4:14,15; 1 Wakorintho 15:1-4; 2 Wakorintho 5:21; Warumi 1:3,4;
Matendo 1:9-11; 1 Timotheo 6:14,15; Tito 2:13;
1 Petro 1:18,19; 2:24
Rejea
KUHUSU ROHO MTAKATIFU
Twaamini kwamba Roho Mtakatifu ni mmoja na Mungu Baba na Mwana
wa Mungu. Aingia kila Mkristo dakika ile amwaminipo Yesu Kristo.
Anawapa Wakristo nguvu na ufahamu wa mambo ya kiroho, na
kuongoza Mkristo katika njia ya haki. Anampa kila Mkristo kipawa
cha kutumia katika kanisa. Kama Wakristo tunapaswa kuenenda
chini ya utawala wake kila siku.
Warumi 8:9; 2 Wakorintho 3:17; Yohana 16:7-13; 14:16,17; Matendo
1:8; Waefeso 1:13,14; 4:30; 5:18, Wagalatia 5:25; 1
Wathesalonike 5:19
Rejea
KUHUSU BIBLIA
Twaamini kwamba Biblia ni Neno la Mungu kwetu sisi. Iliandikwa
na waandishi wanadamu wakiongozwa na Roho Mtakatifu. Twaamini
kwamba Biblia yenyewe ndiyo hiyo iliyo kuu na inayopasa
kukubaliwa na watu wote katika imani na maisha. Kwa sababu ni
yenye pumzi ya Mungu, Biblia ni kweli tupu, bila mchanganyiko
wowote wa kosa.
2 Timotheo 3:16,17; 2 Petro 1:20,21; 2 Timotheo 1:13; Zaburi
119:105,160; Mithali 30:5
Rejea
KUHUSU WANADAMU
Twaamini kwamba mwanadamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu, kusudi
afanane na Mungu na tabia zake. Mwanadamu aliumbwa na Mungu ili
kutawala viumbe vyote na kumletea Mungu sifa na utukufu.
Twaamini kwamba mwanadamu alimwasi Mungu akitaka kujitawala, na
hali hiyo ya uasi na kuepa utawala wa Mungu inaitwa dhambi. Hali
hiyo ya dhambi ndiyo inayowatenga wanadamu na Mungu na kumletea
mwanadamu shida za maishani mwake.
Mwanzo 1:27; 2:17; Zaburi 8:3-6; 51:5; 58:3; Warumi 1:20; 3:23;
5:12-21
Rejea
KUHUSU WOKOVU, KARAMA YA MUNGU
Wokovu ni zawadi ya Mungu kwetu sisi, lakini lazima tupokee
zawadi h iyo. Haiwezekani kujipatia zawadi hiyo kwa njia ya
matendo mema wala yoyote tunayoweza kufanya sisi, bali
inawezekana kwa njia moja tu, kwa njia ya Yesu Kristo. Kwa
kumwamini Yesu Kristo na kukubali kwamba Yeye alijitoa kwa ajili
ya dhambi zetu, ndivyo tunavyoweza kusamehewa na kuokolewa na
adhabu ya dhambi. Tukiamua kuacha nia ya kujitawala na kumgeukia
Yesu katika imani, sisi tunaokolewa. Wokovu huo tunaopata ni wa
milele na huanza papo hapo tunapomkubali Yesu kama Mwokozi.
Yohana 1:12; 3:3; 5:24; 14:6; Warumi 6:23; 5:1; Wagalatia
3:24-26; Waefeso 2:8,9;
1 Yohana 5:13
Rejea
KUHUSU UZIMA WA MILELE
Kwa sababu uzima tunaopata katika Yesu Kristo ni wa milele,
mwaamini anaweza kuwa na uhakika na wokovu siku zote. Baada ya
kuokoka haiwezekani kamwe kupotea tena. Wokovu ni jambo
alilotenda Mungu kwa nguvu zake na neema zake, kwa hivyo si kwa
nguvu za mwaamini anavyoweza kuendelea na wokovu. Ni kwa nguvu
na neema za Mungu na hivyo tunao uhakika kwamba wokovu wetu ni
wa milele kama Biblia inavyosema.
Yohana 10:29; 2 Timotheo 1:12; Waebrania 7:25; 10:10,14; 1 Petro
1:3-5
Rejea
KUHUSU MAMBO YAJAYO
Watu waliumbwa na Mungu ili kuishi milele. Baada ya maisha haya
na kuaga dunia tutaendelea kuishi. Aidha tutaishi tukiwa
tumetengwa na Mungu kwa sababu ya dhambi, ama tutaishi pamoja na
Mungu hata milele, kwa sababu ya msamaha wa dhambi na wokovu
katika Kristo. Kwa hao wasiookoka watakwenda mahali palipoitwa
Jehanum. Kwa hao waliookoka watakwenda kuishi mahali palipoitwa
Mbinguni.
Yohana 3:16,36; Yohana 14:17; Warumi 6:23; Warumi 8:17-18;
Ufunuo 20:15;
1 Wakorintho 2:7-9
Rejea |
|