| |
MSIMAMO WETU
BIBLIA NI MAMLAKA YETU YA PEKEE Timotheo 3:16
Kwa sababu Biblia ni Neno la Mungu kwetu sisi na inaweza
kutegemewa kabisa kama kweli halisi, tunakubali Biblia iwe neno
la mwisho katika maisha yetu. Tunapokabiliwa na shida ama swali,
kwanza tunauliza “Biblia inasemaje?” Tunafundisha waamini kusoma
Biblia kila siku, kujifunza Biblia, na kuweka mistari ya Biblia
moyoni ili waweze kuitafakari na kuikariri. Biblia ndiyo asili
ya imani yetu na mazoea yetu.
Rejea
KILA KANISA LAJISIMAMIA
Wakolosai 1:18
Kristo ndiye kichwa cha kanisa letu. Si mtu, si kamati, wala si
dhehebu fulani. Ingawa tunashirikiana na kusaidiana na makanisa
mengine mara kwa mara, tunaamini kwamba kila kanisa linapaswa
kujisimamia, kujitegemea, na kufanya kama linavyoongozwa na
Kristo aliye Kichwa. Hakuna dhehebu wala wakubwa waliopewa
mamlaka yoyote juu ya kanisa letu.
Rejea
KILA MWAMINI NI KUHANI
Ufunuo 1:5,6; 1 Petro 2:9
Biblia inatufundisha kwamba kila mwamini anaweza kumkaribia
Mungu kwa njia ya sala na kusoma Biblia, na hakuna haja ya
kuhani mpatanishi. Pia, Biblia inafundisha kwamba kila Mkristo
anaitwa kufanya kazi ya Mungu. Labda mmoja ni fundi gari, na
mwingine ni mwalimu, lakini kanisani sisi sote tumeitwa kutumia
karama yetu ya kiroho na kufanya huduma. Katika kanisa letu sisi
husihi kila mwamini kufanya huduma na hivyo kufanya kazi ya
Mungu.
Rejea
KILA MSHIRIKA ATOE ZAKA
Mambo Ya Walawi 27:30
Katika kanisa letu waamini wanafundishwa kutoa zaka kwa ajili ya
kanisa na kazi ya Mungu. Kutoa zaka (asilimia 10 ya mapato yote)
ni amri ya Mungu na ndio msingi wa kutoa kwetu.
Rejea
KUBATIZWA KWA MAJI MENGI
Wakolosai 2:12
Tunabatiza kwa njia moja tu, kwa njia ya maji mengi. Hiyo ndiyo
jinsi alivyobatizwa Yesu na ndiyo njia ya pekee katika Biblia.
Rejea
KUONGOZWA NA ROHO
MTAKATIFU Yohana 15:5
Tunaamini kwamba Mkristo anahitaji nguvu ya Roho Mtakatifu ili
kuishi maisha yampendezayo Mungu. Tunajitahidi kumtegemea Mungu
na Roho wake kila siku ili kutenda yaliyo haki. (Wafilipi 2:13;
Waefeso 5:18)
Rejea
KUWAAMBIA
WENGINE HABARI ZA KRISTO 1 Petro 3:15
Ni wajibu wa kila Mkristo kuwaambia wengine habari njema ya Yesu
Kristo. Hivyo waamini wa kanisa letu wanasihiwa kuwashuhudia
wengine na kuwakaribisha majirani, jamaa, na marafiki katika
vipindi na ibada za kanisa.
Rejea |
|