Msimamo Wetu


Karibu

Ibada Zetu

Huduma Zetu

Mahali Tulipo

Kusudi Letu

Imani Yetu

Uongozi Wetu

Wamisionari
Wetu

Wasiliana Nasi

Niambie Zaidi
Juu Ya Wokovu!

English

 

MSIMAMO WETU

BIBLIA NI MAMLAKA YETU YA PEKEE Timotheo 3:16
Kwa sababu Biblia ni Neno la Mungu kwetu sisi na inaweza kutegemewa kabisa kama kweli halisi, tunakubali Biblia iwe neno la mwisho katika maisha yetu. Tunapokabiliwa na shida ama swali, kwanza tunauliza “Biblia inasemaje?” Tunafundisha waamini kusoma Biblia kila siku, kujifunza Biblia, na kuweka mistari ya Biblia moyoni ili waweze kuitafakari na kuikariri. Biblia ndiyo asili ya imani yetu na mazoea yetu.
Rejea

KILA KANISA LAJISIMAMIA Wakolosai 1:18
Kristo ndiye kichwa cha kanisa letu. Si mtu, si kamati, wala si dhehebu fulani. Ingawa tunashirikiana na kusaidiana na makanisa mengine mara kwa mara, tunaamini kwamba kila kanisa linapaswa kujisimamia, kujitegemea, na kufanya kama linavyoongozwa na Kristo aliye Kichwa. Hakuna dhehebu wala wakubwa waliopewa mamlaka yoyote juu ya kanisa letu.
Rejea

KILA MWAMINI NI KUHANI Ufunuo 1:5,6; 1 Petro 2:9
Biblia inatufundisha kwamba kila mwamini anaweza kumkaribia Mungu kwa njia ya sala na kusoma Biblia, na hakuna haja ya kuhani mpatanishi. Pia, Biblia inafundisha kwamba kila Mkristo anaitwa kufanya kazi ya Mungu. Labda mmoja ni fundi gari, na mwingine ni mwalimu, lakini kanisani sisi sote tumeitwa kutumia karama yetu ya kiroho na kufanya huduma. Katika kanisa letu sisi husihi kila mwamini kufanya huduma na hivyo kufanya kazi ya Mungu.
Rejea

KILA MSHIRIKA ATOE ZAKA Mambo Ya Walawi 27:30
Katika kanisa letu waamini wanafundishwa kutoa zaka kwa ajili ya kanisa na kazi ya Mungu. Kutoa zaka (asilimia 10 ya mapato yote) ni amri ya Mungu na ndio msingi wa kutoa kwetu.
Rejea

KUBATIZWA KWA MAJI MENGI Wakolosai 2:12
Tunabatiza kwa njia moja tu, kwa njia ya maji mengi. Hiyo ndiyo jinsi alivyobatizwa Yesu na ndiyo njia ya pekee katika Biblia.
Rejea

KUONGOZWA NA ROHO MTAKATIFU Yohana 15:5
Tunaamini kwamba Mkristo anahitaji nguvu ya Roho Mtakatifu ili kuishi maisha yampendezayo Mungu. Tunajitahidi kumtegemea Mungu na Roho wake kila siku ili kutenda yaliyo haki. (Wafilipi 2:13; Waefeso 5:18)
Rejea

KUWAAMBIA WENGINE HABARI ZA KRISTO 1 Petro 3:15
Ni wajibu wa kila Mkristo kuwaambia wengine habari njema ya Yesu Kristo. Hivyo waamini wa kanisa letu wanasihiwa kuwashuhudia wengine na kuwakaribisha majirani, jamaa, na marafiki katika vipindi na ibada za kanisa.
Rejea

 
 

Updated 03 May 2008